1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Mataifa kupeleka jeshi Kongo

Admin.WagnerD19 Julai 2013

Umoja wa Mataifa umesema upo tayari kupeleka jeshi katika uwanja wa mapambano huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo kukabiliana na Waasi. Hatua inayotokana na malalamiko ya waandamanaji mjini Goma.

https://p.dw.com/p/19Afs
Congolese Army soldiers man a foward position in Kanyarucinya, some 12 kms from Goma, in the east of the Democratic Republic of the Congo on July 16, 2013. The army in the Democratic Republic of Congo on July 16 pursued an offensive against rebels of the M23 movement to protect the North Kivu provincial capital of Goma. M23, a movement launched by Tutsi defectors from the army who accuse the Kinshasa government of reneging on a 2009 peace deal, last year occupied Goma for 10 days before pulling out under international pressure. AFP PHOTO / PHIL MOORE (Photo credit should read PHIL MOORE/AFP/Getty Images)
Kämpfe im OstkongoPicha: Phil Moore/AFP/Getty Images

Waandamanaji wanalalamika kwamba walinzi wa amani wamekuwa dhaifu katika kukabiliana na vitendo vya waasi katika maeneo hayo.

Jeshi la Umoja wa Mataifa nchini Kongo limeonekana kujiweka kando kabisa wakati wapiganaji waasi wa kundi la M23 likifanya mashambulizi dhidi ya majeshi ya serikali katika eneo kubwa la mashariki la mji wa Goma.

Msemaji wa Umoja wa Mataifa Martin Nersirky amenukuliwa na shirika la habari la Ufaransa, AFP akisema jeshi la ulinzi wa amani nchini Kongo, MONUSCO  kwa wakati wote katika operesheni zake nchini humo halijajiingiza katika uhasama.

Jeshi lipo katika hali ya tahadhari

Msemaji huyo ameongeza kusema majeshi ya bado yapo katika hali ya tahadhari na kujitayarisha kujiingiza katika mapigano hayo, kwa kujumuisha jeshi jipya kwa lililopo nchini humo kwa hivi sasa kwa ajili ya kuleta ustawi. Amesema operesheni hiyo inaweza kuwaweka katika hali ya wasiwasi wakazi wa eneo hilo la mashariki ya Kongo, na hasa Goma.

A Congolese army soldier walks through the bush, back from an attack position north-west of Munigi, overlooking the front-line, in the east of the Democratic Republic of the Congo on July 15, 2013. Fighting broke out yesterday between M23 rebels and the national army, and continued today, with heavy artillery fire north-west of Munigi and the army claiming to have taken ground. AFP PHOTO/PHIL MOORE (Photo credit should read PHIL MOORE/AFP/Getty Images)
Mwanajeshi wa Kongo kwenye doria katika viunga vya GomaPicha: Phil Moore/AFP/Getty Images

Kwa mujibu wa AFP, tangu jana kumekuwa kimya katika eneo la Goma. Lakini kulikuwa na maandamano katika mji huo, ambapo baadhi ya wamelituhumu jeshi hilo la Umoja wa Matiafa kwa kutotoa ushirikiano wa kutosha kwa majeshi ya serikali ya Kongo.

Doria yaendelea Goma

Hadi sasa kuna wanajeshi 2,000 kutoka Afrika Kusini, kati ya 3,000 wanaounda jeshi hilo la Umoja wa Mataifa. Idadi iliyobaki kati ya hao inatoka Tanzania na Malawi. Majeshi hayo yanafanya tu, doria na kwamba mpaka sasa hawajafanya shambulizi lolote pamoja na kuwa na mamlaka ya kufanya hivyo kama inavyoelekeza mamlaka waliopewa na baraza la usalama la Umoja wa Mataifa.

Msemaji wa Umoja huo Nesirky amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesikitishwa sana uhasama mpya katika maeneo ya mji mkuu wa Kivu ya Kaskazini. Kiongozi huyo wa ametaka pande zote husika katika eneo hilo kufanya jithada katika kudhibiti kuongeka kwa mogogoro huo ambao utazidisha matatizo kwa wakazi.

Waasi wa M23 walifanya mashambulizi Jumapili iliyopita ambapo Jeshi la Kongo lilisema kiasi ya watu 130, waliuwawa.

Mwandishi: Sudi Mnette/AFP
Mhariri:Yusuf Saumu