1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umwagaji damu usitishwe Syria

Martin, Prema/afpe21 Januari 2012

Umoja wa Nchi za Kiarabu unashinikizwa kuomba msaada wa Umoja wa Mataifa huku sauti zikizidi kupazwa kuwa tume iliyopelekwa Syria hivi karibuni, imeshindwa kuzuia mauaji yanayoendelea tangu miezi kumi nchini humo.

https://p.dw.com/p/13nW5
epa03046146 A handout picture released by Syrian Arab news agency SANA, shows Arab League observers in orange jackets upon their arrival to check wounded people in the national hospital in Daraa southern Syria 31 December 2011. According to media reports on 31 December, Arab League peace observers, inspecting hotspots across Syria, have called on the government to remove 'immediately' snipers from rooftops of buildings. The observers are in Syria to verify the government's compliance with an Arab League peace plan, which includes removing military hardware from civilian areas and releasing detainees from prisons. More than 5,000 people have been killed in the Syrian government's crackdown on a pro-democracy uprising since it started in mid-March, according to the United Nations. EPA/SANA HANDOUT HANDOUT EDITORIAL USE ONLY/NO SALES +++(c) dpa - Bildfunk+++
Tume ya waangalizi wa Umoja wa Nchi za Kiarabu nchini SyriaPicha: picture-alliance/dpa

Licha ya tume ya umoja huo kukosolewa vikali, naibu mkuu wa operesheni za tume hiyo ya waangalizi, Ali Jarush amewaambia waandishi habari kuwa muda wa tume hiyo, huenda ukarefushwa kwa mwezi mmoja. Wakati huo huo, mkuu wa tume ya waangalizi, Jenerali Mohammed Ahmed Mustafa al-Dabi kutoka Sudan, anajiandaa kuwasilisha ripoti ya tume hiiyo kwa mawaziri wa mambo ya nje wa nchi za Kiarabu, wanaokutana mjini Cairo siku ya jumapili, kujadili hatua inayofaa kuchukuliwa.

Demonstrators protest against Syria's President Bashar al-Assad in Zabadani, near Damascus Januray 13, 2012. The banner reads, "Go, want to back to my school". REUTERS/Handout (SYRIA - Tags: POLITICS CIVIL UNREST) FOR EDITORIAL USE ONLY. NOT FOR SALE FOR MARKETING OR ADVERTISING CAMPAIGNS. THIS IMAGE HAS BEEN SUPPLIED BY A THIRD PARTY. IT IS DISTRIBUTED, EXACTLY AS RECEIVED BY REUTERS, AS A SERVICE TO CLIENTS
Wapinzani wa Rais Bashar al-Assad wakiandamana nje ya mji mkuu DamascusPicha: Reuters

Lakini shirika linalotetea haki za binadamu "Human Rights Watch" linasema, kuwepo kwa tume hiyo ya Umoja wa nchi za Kiarabu huko Syria, wala haikusaidia kukomesha ukandamizaji unaofanywa na serikali ya nchi hiyo. Wanaharakati wanasema, tangu tume hiyo ya waangalizi ilipokwenda Syria Desemba 26, raia 506 wameuawa na wengine 490 wametiwa mbaroni. Sasa, Umoja wa Nchi za Kiarabu unahimizwa na shirika la "Human Rights Watch" kutamka hadharani kuwa Syria haikuheshimu mpango wa umoja huo.

Kwa hivyo, umoja huo sasa ndio uanze kushirikiana na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuishinikiza serikali ya Syria na matumizi ya nguvu yasite. Mkuu wa Baraza la kitaifa la Syria (SNC), linalojumuisha makundi ya upinzani, Burhan Ghaliun amekwenda Cairo nchini Misri, kuwashawishi mawaziri wa nchi za Kiarabu kuiwasilisha ripoti ya tume ya waangalizi katika Baraza la Usalama ili hatua kali ipate kuchukuliwa. Wakati huo huo, shirika rasmi la habari la Misri, MENA limeripoti kuwa Ahmed el-Tayyeb, Imam mkuu wa Al-Azhar - kituo kikuu cha masomo ya Kiislamu mjini Cairo, amewahimiza viongozi wa Kiarabu kuchukua hatua zinazohitajika kusitisha umwagaji damu nchini Syria.

epa03016900 (L-R)Arab League Secretary General Nabil Alarabi ,Qatari Foreign Minister Hamad bin Jasim ,Turkey's Foreign Minister Ahmet Davutoglu , Egyptian Foreign Minister Mohamed Kamel Amr attend the Arab Foreign Ministers emergency meeting about Syria,in Cairo, Egypt, 27 November 2011. Arab League Foreign Ministers meet in Cairo later on 27 November to decide whether to rubber-stamp a set of sanctions on Syria drafted by their Economy Ministers after Damascus ignored a deadline designed to end its violent crackdown on protesters. Qatari Foreign Minister Hamad bin Jassim, who heads the league's ministerial committee on Syria, arrived in Cairo early Sunday. Turkish Foreign Minister Ahmet Davutoglu was also expected to take part in the talks. On 26 November, its Economy Ministers drafted a set of sanctions, which include a ban on travel by senior Syrian officials and the suspension of trade links. EPA/KHALED ELFIQI +++(c) dpa - Bildfunk+++
Mawaziri wa Kiarabu watafuta ufumbuzi wa mzozo wa SyriaPicha: picture-alliance/dpa

Kwa upande mwingine, waandamanaji wa Kisyria walioghadhibika, walikusanyika nje ya ubalozi wa Urusi mjini Cairo kutoa dukuduku lao kuhusu msimamo wa nchi hiyo kuiunga mkono serikali ya Rais Bashar al-Assad wa Syria. Urusi na China zenye kura turufu katika Baraza la Usalama, zilipinga azimio lililopendekeza kuchukuliwa hatua kali dhidi ya Syria. Mkwamo huo katika Baraza la Usalama humaanisha kuwa sasa viongozi wa Kiarabu ndio wanazidi kushinikizwa kutafuta suluhisho la mzozo wa Syria. Umoja wa Mataifa unatathmini kuwa zaidi ya watu 5,400 wameuawa katika ukandamizaji ulioanza mwezi Machi nchini Syria.

Mwandishi: Martin, Prema/afpe
Mhariri: Alakonya, Bruce