1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiTunisia

Usafiri wasimama Tunis, kufuatia mgomo wa watumishi

2 Januari 2023

Shughuli za uchukuzi wa umma katika mji mkuu wa Tunisia, Tunis, zimetatitizika pakubwa leo Jumatatu baada ya wafanyikazi wa kampuni ya usafiri wa umma kufanya mgomo.

https://p.dw.com/p/4LeK3
Tunesien Flagge auf dem Justizpalast in Tunis
Picha: Thierry Monasse/dpa/picture alliance

Wafanyakazi hao wamegoma kutokana na ucheleweshwaji wa malipo na marupurupu.

Msemaji wa kampuni hiyo ya usafiri Hayat Chamtouri, amesema muungano wa wafanyikazi unapinga kucheleweshwa kwa malipo na marupuru ya wafanyikazi.

Mgomo huo umeweka wazi matatizo ya kifedha yanayozikabili kampuni za umma ambazo ziko ukingoni mwa kufilisika, wakati serikali ya Rais Kais Saied ikiwa inakumbwa na mzozo mbaya wa kifedha.

Mgomo huo wa usafiri ni ishara ya nguvu ilizo nazo muungano huo wa wafanyikazi wa UGTT, ambao umeahidi kuendelea kuishinikiza serikali.

Muungano huo wa wafanyikazi, wenye wanachama milioni 1, umeidhinisha siku mbili za mgomo katika sekta ya uchukuzi ikiwemo safari za ndege, nchi kavu na baharini kuanzia Januari 25 na 26, ili kupinga kile walichokiita "serikali kutelekeza baadhi ya kampuni za umma."