1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

VATICAN: Afisa wa polisi ajiua

3 Septemba 2007
https://p.dw.com/p/CBSy

Afisa wa polisi mjini Vatican Italia, amekufa kutokana na majeraha ya risasi katika tukio linalochukuliwa kuwa hatua ya afisa huyo kujiua mwenyewe.

Taarifa ya Vatican inasema afisa huyo mwenye umri wa miaka 25 alipatikana akiwa katika hali mbaya ndani ya bafu ya kambi yao mapema leo na kupelekwa hospitalini, ambako alikufa muda mfupi baadaye.

Wachunguzi wa Vatican wanachunguza ujumbe katika barua aliyowachwa na afisa huyo.

Tukio hilo limeleezwa kuwa baya kuwahi kutokea ndani ya makao ya Vatican tangu mwaka wa 1998 wakati afisa wa kikosi cha usalama cha Swiss Guard alipomuua kamanda wake na mke wa kamanda huyo kabla kujipiga risasi na kujiua.