1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Vienna. Iran na IAEA zafikia makubaliano.

14 Julai 2007
https://p.dw.com/p/CBiy

Shirika la umoja wa mataifa la nishati ya atomic limesema kuwa limefikia makubaliano na Iran ambayo yanatatua masuala yaliyobaki juu ya majaribio ya hapo kabla ya Plutonium ya nchi hiyo.

Kufuatia mazungumzo ya siku mbili mjini Tehran , shirika hilo la kimataifa la nishati ya Atomic limesema kuwa limepanga wachunguzi wa IAEA kutembelea kinu cha kinuklia cha utafiti wa maji maji mazito katika eneo la Arak ifikapo mwishoni mwa mwezi Julai.

Uamuzi juu ya kushughulikia usalama katika kinu cha urutubishaji wa madini ya Uranium katika kituo cha Natanz unatarajiwa kufikiwa mapema mwezi wa August.

Mataifa ya magharibi yanashaka kuwa mpango wa kinuklia wa Iran ni wa kuunda silaha za kinuklia. Iran inasema kuwa inataka teknolojia hiyo ya kinuklia kwa ajili ya kuzalisha umeme.