1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Vijana wa Mashariki ya Ujerumani miaka 20 baada ya muungano

Benjamin Hammer3 Oktoba 2010

Vijana wa Ujerumani ya mashariki hawaoni tofauti kati yao na wenzao wa Ujerumani magharibi. Kwa hiyo wanakulia katika Ujerumani tofauti kabisa. Wengi wangependa kuhamia katika shule za upande wa Ujerumani magharibi.

https://p.dw.com/p/PRzc
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Karl-Liebknecht, mjini Frankfurt OderPicha: Benjamin Hammer

Tarehe 3 mwezi wa Oktoba mwaka huu yaani Jumapili ijayo, Ujerumani itaadhimisha miaka 20 ya Muungano kati ya Mashariki na Magharibi. Jee  hali ikoje katika maisha ya vijana hivi sasa. Vijana kutoka  eneo la  Ujerumani  ya  mashariki hawaoni  tofauti  kati yao   na  wenzao wa eneo la  Ujerumani  magharibi. Kwa  hiyo wanakulia  katika  Ujerumani  tofauti  kabisa. Wengi  wangependa kuhamia  katika   shule   za  upande  wa   Ujerumani  magharibi. Sekione Kitojo anawasimulia zaidi.

Frankfurt  an der Oder:  Kwa  Wajerumani  ya  mashariki  wengi zaidi  si  jambo  linalowezekana,  kwa  upande  wa  kijiografia. Mji huo  uko mkabala  na  mpaka  na  Poland. Kwa  wengi  wa  watu  wa Ujerumani  ya  magharibi  hii  ina  maana  ya  kuongezeka  kwa  watu wasio  na  ajira  na  kuporomoka  kwa  mambo. Wanafunzi  wa  shule ya  sekondari  ya  Karl-Liebknecht  wanakerwa  na  dhana  kama hiyo. Kwa  kuwa  mtu  yeyote  anayeripoti  kuhusu  sisi, anazungumzia  tu  kuhusu  ukosefu  wa  ajira  ama  watu  wenye msimamo  mkali, anasema  Florian Hundertmark  mwenye  umri  wa miaka  17. Kwa  hiyo  mtu  hawezi  kuwaona   kwa  mtazamo  mzuri  , watu  wa  magharibi  kutoka  Frankfurt.

Florian  anaishi   na  Käthe mwenye  umri  wa  miaka  18  na  Jörn , mwenye  umri  wa  miaka  16  katika   kitongoji  cha  Oder. Vijana hao  wanasoma  katika  madarasa  ya  juu  katika  shule  hiyo  ya sekondari.   Upande  wa  pili  nchini  Poland , kuna  mji   wa  Slubice, si  mbali  sana  na  inaweza  kusikika   kengele  ya  kanisa  la  Maria. Kwa  kweli  hapa  mtu  anaweza  kufanya  kila  kitu  anachopenda. Ni mahali  pazuri  sana , anasema  Jörn. Lakini  watu   wanahamia sehemu  nyingine.

Wakati  vijana  kutoka  Frankfurt  an der Oder  wakikumbuka   kuhusu muungano  wa  nchi  mbili  za  Ujerumani, kuhusu  Ujerumani magharibi,  haliji    suala  la  kisiasa  ama  historia. Linakuja  suala hali  yao  ya  baadaye  katika  soko  la  kazi.  Kiwango  cha  ukosefu wa  ajira  katika  Ujerumani  mashariki  unafikia  asilimia 11.5, ambapo ni karibu  mara  mbili  kuliko  Ujerumani ya magharibi. Mwaka  1990  mjini  Frankfurt  kulikuwa  na  watu 88,000. Miaka  20 baadaye  mabadiliko  yamesababisha  watu  karibu  30,000 kuuhama  mji  huo. Hata  Käthe, Jörn  na  Florian  wanataka kuhamia  katika   majimbo  mengine  ya  Ujerumani. Florian  anataka kusomea  kuhusu  utengenezaji  wa  magari, mafunzo  hayo yanapatikana  tu  upande  wa  magharibi, anasema.  Ndio  sababu ningependa   sana  kubakia  katika  maeneo  haya  ya  karibuni.

Miaka  20  baada  ya  muungano  kumekuwa  na   tofauti   ya kiuchumi  kati  ya  vijana  wa  mashariki  na  magharibi. Vinginevyo wanakubaliana  vijana  hao  wote, kwamba  Ujerumani  haikugawika, anahisi  Jörn. Mtu  anasikia  kila  mara  kuhusu  ukuta, lakini  nafikiri , taratibu  hilo  linaondoka. Wanafunzi  hao  wa  madarasa  ya  juu wanaifahamu  Ujerumani    kuwa ni  nchi  tu  iliyoungana. Wamezaliwa  kati  mwaka  1992  na  1994.

Kundi  la  muziki   maarufu  walipendalo, kilabu  ya  michezo,  likizo katika  eneo  la  Mallorca,  ni  masuala   ya  kitamaduni yanayowashughulisha  vijana  hawa, ambao kiuhalisi    wamekua kama  vijana  wa  Ujerumani. Anaona   hivyo  pia  Thomas   kutoka katika   taasisi  ya  utafiti  ya  TNS  Infratest.

Ukilinganisha   kizazi  cha   watu  wa  mashariki  na  magharibi , unaweza  kusema  kundi  hili  la  vijana  ndio  la  kweli, anasema Gensicke. Mtafiti  huyo  alizaliwa  katika  mji  wa  Magdenburg upande  wa  mashariki  na  akahamia  Ujerumani  ya  magharibi baada  ya  muungano. Historia  yake  inamfanya  kuwa  katika nafasi  ya  kutazamwa  katika masuala  aliyosomea  ya  sayansi.

Kwa  hali  yoyote  ile,  kuna  tofauti, anasema  Gensicke.  Vijana katika  Ujerumani  mashariki  wanautilia  shaka   mfumo  wa  kisiasa. Wakati  tunapowauliza  vijana , iwapo  wanaona  demokrasia inafanyakazi  vizuri, utawaona  vijana  wengi  wa  mashariki  wakitoa hoja  za  umuhimu  wa  kufanyia  mageuzi. Kuhusiana  na  hilo wanamaana  hata  upande  wa  Ujerumani  magharibi. Na  hali  hii  ni mpya  pia  kwa  upande  wa  mashariki.

Je mtazamo  huu   wa  ukosoaji  unaleta  changamoto  kwa   nchi nzima? Hapana,  wanasema   wanafunzi  hao  la  shule  ya sekondari  ya  Liebknecht. Tumeridhika, kwamba   kuna  umoja, anasema  Inka  Sörries  wa   kidato  cha  12. Katika  upande  wa mashariki   kuna  uhuru  ambao  unamipaka  mingi, kwa  mfano marufuku  ya  kusafiri  nje.

Ossis, Wessis,  ikiwa  na  maana  wamashariki  na  wamagharibi, maneno haya  yanajitokeza  kila  mara. Na ni kwasababu yanatumiwa   kama  maneno tu ya utani  kwa  vijana  wa  shule, ambao wamehamia  baada  ya  muungamo na wazazi  wao   mjini Frankfurt. Miaka  miwili nyuma   walikutana   nchini  Ufaransa  na vijana  wawili  kutoka   katika   majimbo ya   Bayern  na  Hessen, anasema  Käthe. Walikuwa wanafahamu  mjini  wa  Frankfurt/Oder uko  wapi.