1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Vikosi vya Ouattara vyayashikilia makaazi ya Gbagbo

Mohammed Khelef5 Aprili 2011

Vikosi vinavyomtii raisi wa Cote d'Ivoire anayetambuliwa kimataifa, Alassane Ouattara, vimeripotiwa kudhibiti makaazi ya rais anayeng'ang'ania madaraka, Laurent Gbagbo, na bado Gbagbo mwenyewe hajuilikani alipo.

https://p.dw.com/p/10naJ
Laurent Gbagbo
Laurent GbagboPicha: picture alliance/landov

Msemaji wa waasi amesema kuwa vikosi vya Ouattara vinafanya msako kwenye majengo yaliyo jirani na makaazi hao ya raisi.

Bado haijafahamika ikiwa uvamizi huu umefanikiwa kumnasa Gbagbo, ambaye ameendelea kung'ang'ania madaraka licha ya wito wa kimataifa wa kumtaka aondoke.

Wakati huo huo, helikopta za Umoja wa Mataifa zimeishambulia kambi ya wanajeshi wa Gbagbo mjini Abdijan hapo jana. Vikosi vya Ufaransa vilishiriki pia kwenye operesheni hii yenye lengo la kuziharibu silaha nzito kwenye kambi za vikosi vya Gbagbo.

Umoja wa Ulaya umeunga mkono juhudi za Umoja wa Mataifa, huku Rais wa Umoja huo, Herman Van Rompuy, akisema kuwa ni lazima Gbagbo aondoke madarakani ili imani ipatikane.