1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Viongozi wa dunia kuhutubia baraza kuu la umoja wa mataifa

24 Septemba 2012

Vita nchini Syria ,hali ya wasi wasi inayoongezeka kuhusiana na mpango wa Iran wa kinuklia na maandamano ya Waislamu dhidi ya mataifa ya magharibi, vitaweka kiwingu katika mkutano wa umoja wa mataifa.

https://p.dw.com/p/16Cro
The General Assembly today adopted a resolution condemning the increasing use of heavy weapons by Syrian authorities and urging all sides of the conflict to immediately cease armed violence. The resolution, presented by the Arab Group, was adopted by a vote of 133 in favour to 12 against with 31 abstentions. Seated at the podium are Nassir Abdulaziz Al-Nasser (left) President of the sixty-sixth session of the General Assembly, and Ion Botnaru, Director of the General Assembly and the Economic and Social Council (ECOSOC) Affairs Division. 03 August 2012 United Nations, New York Photo # 522522 Copyright: UN via Nina Werkhäuser, DW Hauptstadtstudio
Baraza kuu la umoja wa mataifa kuanza mkutano wake JumannePicha: UN

Maneno ya tahadhari pamoja na ukaidi yanatarajiwa wakati rais wa Marekani Barack Obama , kiongozi wa Iran Mahmoud Ahmedinejad na waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu watakapojiunga na zaidi ya viongozi 120 wa mataifa na serikali katika baraza kuu la umoja wa mataifa.

Kwa sababu ya mgawanyiko mkubwa wa kimataifa kuhusiana na mzozo uliodumu sasa miezi 18 nchini Syria , umoja wa mataifa hautakuwa na mkutano rasmi kuhusiana na vita hivyo vya wenyewe kwa wenyewe.

Obama kuhutubia kwanza

Lakini rais Obama na viongozi wa mataifa ya magharibi wanatarajiwa kutoa wito wa kuchukuliwa hatua katika hotuba zao. Rais wa Marekani ni mmoja kati ya wazungumzaji wa mwanzo siku ya Jumanne asubuhi baada ya tukio hilo kufunguliwa na katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki-moon.

U.N. Secretary General Ban Ki-moon addresses the 66th session of the United Nations General Assembly, Wednesday, Sept. 21, 2011. (Foto: AP) // Eingestellt von wa
Katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki MoonPicha: AP

Na kampeni dhidi ya Syria itaendelezwa nje ya baraza kuu la umoja wa mataifa. Mjumbe wa Umoja wa Mataifa na mataifa ya Kiarabu, Arab League Lakhdar Brahimi atatoa maelezo katika baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kesho Jumatatu kuhusiana na mazungumzo yake na rais Bashar al-Assad.

Syria pia inakuwa mada kuu katika baraza la usalama wakati wa mjadala wa mawaziri kuhusiana na Arab League siku ya Jumatano, umoja wa ulaya unatarajiwa kuanzisha wito mpya kwa ajili ya mfuko wa fedha za huduma ya kiutu na mkutano wa mawaziri wa marafiki wa Syria unapangwa kufanyika siku ya Ijumaa.

Majeraha ya kidiplomasia

Majeraha ya kidiplomasia kuhusu Syria hayako karibu na kupata nafuu. Si Urusi ama China , nchi ambazo zimetumia kura zao za turufu mara tatu kuzuwia maazimio ya baraza la usalama kuhusu Syria , zitawakilishwa na viongozi wa ngazi ya juu mjini New York.

WASHINGTON, DC - SEPTEMBER 12: U.S. President Barack Obama (R) makes a statement about the death of U.S. ambassador to Libya J. Christopher Stevens with Secretary of State Hillary Clinton in the Rose Garden at the White House September 12, 2012 in Washington, DC. Stevens and three other embassy employees were killed when the embassy in Benghazi was attacked by a mob potentially angered by an American-made video mocking Islam's founding prophet. (Photo by Chip Somodevilla/Getty Images)
Rais Barack ObamaPicha: Getty Images

Assad anatarajiwa kumtuma waziri wake wa mambo ya kigeni.

"Kila mmoja atakuwa anafikiri kuhusu Syria, atazungumza kuhusu Syria , lakini hakutakuwa na uamuzi na hakuna hatua kubwa itakayopigwa," amesema mwanadiplomasia mmoja mwandamizi wa umoja wa mataifa, akizungumza kwa mashariti ya kutotajwa jina.

Stewart Patrick , mtaalamu wa taasisi ya kimataifa inayokusanya mawazo kuhusu utawala wa dunia kwa ajili ya baraza la uhusiano wa kimataifa , amesema hata hivyo kuwa Syria itakuwa moja ya masuala yanayopewa umbele katika baraza kuu la umoja wa mataifa pamoja na mvutano kuhusu Iran. Ahmedinejad yuko mjini New York huenda kwa mara yake ya mwisho kuonekana katika baraza kuu.

Wasi wasi wazidi

Hali ya wasi wasi wa usalama pamoja na diplomasia zaidi vinatarajiwa huku kukiwa na uvumi mkubwa kuwa Israel inapanga kuishambulia kijeshi Iran katika maeneo yake ya kinuklia ambapo Iran inasisitiza kuwa ni kwa ajili ya matumizi ya amani, lakini mataifa ya magharibi yanasema nchi hiyo inaficha majaribio ya kutengeneza bomu la nuklia.

Ahmedinejad atazungumza katika baraza kuu siku ya Jumatano, wakati hatua mpya ya mataifa kadha kutoka katika ukumbi huo ikitarajiwa iwapo kiongozi huyo wa Iran atarejea matamshi yake ya kuishambulia Israel.

Iranian President Mahmoud Ahmedinejad flanked by a Turkish, left, and an Iran flag as he poses for cameras before a meetIing with Turkey's Prime Minister Recep Tayyip Erdogan in Istanbul, Turkey, Wednesday, Dec. 22, 2010.(AP Photo/Tolga Bozoglu, Pool)
Rais wa Iran Mahmud AhmadinejadPicha: AP

Maafisa wa ngazi ya juu kutoka Uingereza, China, Ufaransa, Ujerumani, Urusi na Marekani , ambao wanajaribu kujadiliana na Iran, wanatarajiwa kukutana siku ya Alhamis mara tu baada ya waziri mkuu wa Israel Netanyahu kulihutubia baraza kuu la umoja wa mataifa.

Israeli Prime Minister Benjamin Netanyahu gestures as he addresses the weekly cabinet meeting in Jerusalem, Sunday, Sept. 9, 2012. (Foto:Menahem Kahana, Pool/AP/dapd)
Waziri mkuu wa Israel Benjamin NetanyahuPicha: dapd

Obama na Netanyahu

Kushindwa kutayarisha mkutano kati ya Netanyahu na rais Obama kumezusha uvumi kuhusu kuongezeka kwa mpasuko kati ya viongozi hao wawili. Marekani na washirika wake wameongeza juhudi zao za kutoa onyo kwa Iran, hata hivyo , muda unafikia tamati kwa ajili ya kupata suluhisho kuhusiana na mvutano huu.

Netanyahu atahutubia baraza kuu mara baada ya kiongozi wa Palestina Mahmoud Abbas kuhutubia. Mwaka jana kiongozi huyo wa Palestina alikuwa kivutio kikubwa kwa juhudi zake zilizovuta hisia za kutaka kuwa mwanachama kamili wa umoja wa mataifa, juhudi ambazo zimezuiwa na Marekani.

Mwandishi: Sekione Kitojo /afpe

Mhariri: Iddi Ismail Ssessanga