1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Viongozi wa nchi za Kiarabu kukutana Misri

Kabogo Grace Patricia19 Januari 2011

Viongozi wa nchi za Kiarabu wanakutana leo nchini Misri kujadiliana kuhusu biashara na maendeleo. Huo ni mkutano wao kwanza tangu kiongozi wa Tunisia, Zine El Abidine Ben Ali aondolewe madarakani wiki iliyopita.

https://p.dw.com/p/zzQn
Katibu Mkuu wa jumuiya ya nchi za Kiarabu, Amr MoussaPicha: AP

Wakati huo huo, Rais wa Tunisia, Foued Mebazaa na Waziri Mkuu, Mohammed Ghannouchi jana wamejiuzulu kwenye chama tawala katika hatua ya kutimiza matakwa ya wanasiasa wa upinzani na viongozi wa chama kikuu cha wafanyakazi.

Kituo cha televisheni ya taifa kimeripoti kuwa viongozi hao wamebakia katika nafasi zao kama rais na waziri mkuu. Mapema, mawaziri wanne walijiuzulu kutoka katika serikali ya mpito ya Waziri Mkuu Ghannouchi. Wizara muhimu zinaendelea kushikiliwa na wafuasi wa rais wa zamani, Ben Ali.

NO FLASH Tunesien Unruhen Ghannouchi Mbazaa Tunis Regierung
Rais wa mpito wa Tunisia, Foued Mebazaa (Kulia) akiwa na Waziri Mkuu Mohammed GhannouchiPicha: picture alliance/dpa

Utawala wake wa miaka 23 ulimalizika baada ya wiki kadhaa za maandamano kupinga viwango vya umasikini na ukosefu wa ajira nchini humo. Kwenye mji mkuu wa Tunis, jana polisi walitumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji ambao wanataka kuvunjwa kwa chama tawala.