1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wabunge kupiga kura ya kumchagua rais mpya wa Israel

Abdu Mtullya12 Juni 2007

Shimon Peretz yupo bega kwa bega na spika wa zamani Reuven Rivlin katika kutafuta ungwaji mkono kwenye kinya’nganyiro cha uchaguzi war ais utakaofanyika leo hii.

https://p.dw.com/p/CHCl
Shimon Peres anamatumaini ya kuchaguliwa rais mpya
Shimon Peres anamatumaini ya kuchaguliwa rais mpyaPicha: AP

Vyombo vya habari nchini Israel vinafahamisha kuwa Mwanasiasa maarufu nchini humo Shimon Peretz yupo bega kwa bega na spika wa zamani Reuven Rivlin katika kutafuta ungwaji mkono kwenye kinya’nganyiro cha uchaguzi war ais utakaofanyika leo hii.

Shimon Peretz mwenye umri wa miaka 83 na mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel anapambana katika kinyanganyiro cha kuwania kiti cha Urais dhidi ya wagombea wengine wawili akiwemo spika wa zamani Reuven Rivlin wa chama cha mrengo wa kulia cha Likud na Colette Avital wa chama cha mrengo wa shoto kadirifu cha Labour.

Wabunge 120 watapiga kura kwa njia ya siri mchana wa leo kumchagua mrithi wa rais Moshe Katsav anayeandamwa na kashfa ya kumbaka mwanamke.

Kutoka na tuhuma hizo rais Katsav inambidi angatuke madarakani akiwa ni rais wa pili nchini Israel kuondokea wadhifa huo kufuatia fedheha.

Kwa mujibu wa maoni yaliyochapishwa na gazeti moja maarufu nchini humo Peres huenda akajizolea kura 50 huku Rivlin akipata kura 51 na mwisho akawa Avital amabaye huenda akapigiwa kura na wabunge 19 katika duru ya mwanzo.

Ili mgombea kuibuka mshindi katika kinyang’anyiri hicho itambidi kupata kura 61 na endapo hilo halitofanyika basi uchaguzi huo utaingia kwenye duru ya pili ambapo wagombea wawili wa mwanzo watapambana.

Na ikiwa duru ya pili itashindwa kumpata mshindi atakayejinyakulia kura 61 basi duru nyingin e ya tatu itafanyika na yule atakakuwa na kura nyingi zaidi ya mwenzake ndiye atakayekuwa rais mpya.

Peretz aliwahi kugombea nafasi hiyo miaka saba iliyopita na kutegemewa na wengi kwamba angeshinda uchaguzi huo lakini mambo yalikwenda vingine na ushindi huo ukanyakuliwa na Moshe Katsav wa chama cha Likud.

Peretz ni mwanasiasa anayependeza kwa jicho la kimataifa lakini ndani ya Israel amekuwa mtu wa kushindwa katika chaguzi kufuatia kushindwa kukiongoza kupata ushindi chama chake cha Labour kwenye chaguzi za bunge miaka ya 1977,1981,1984,1988,1996.

Vile vile ameshindwa mwaka 2000 katika uchaguzi war ais dhidi ya bwana Katsav na pia mwaka 2005 alikosa kupata ushindi wa kuongoza chama cha Labour ambapo baadaye aliamua kujitoa na kuingia kwenye chama kipya cha Kadima kilichoundwa na waziri mkuu wa zamani Ariel Sharon. Peretz amewahi kushikilia nyadhifa za waziri wa mambo ya nje na ulinzi nchini Israel.

A mezaliwa Poland mwaka 1923 na ana mke na watoto watatu na wajukuu kadhaa.

Vyombo vya habari nchini Israel vinafahamisha kuwa Mwanasiasa maarufu nchini humo Shimon Peretz yupo bega kwa bega na spika wa zamani Reuven Rivlin katika kutafuta ungwaji mkono kwenye kinya’nganyiro cha uchaguzi war ais utakaofanyika leo hii.

Shimon Peretz mwenye umri wa miaka 83 na mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel anapambana katika kinyanganyiro cha kuwania kiti cha Urais dhidi ya wagombea wengine wawili akiwemo spika wa zamani Reuven Rivlin wa chama cha mrengo wa kulia cha Likud na Colette Avital wa chama cha mrengo wa shoto kadirifu cha Labour.

Wabunge 120 watapiga kura kwa njia ya siri mchana wa leo kumchagua mrithi wa rais Moshe Katsav anayeandamwa na kashfa ya kumbaka mwanamke.

Kutoka na tuhuma hizo rais Katsav inambidi angatuke madarakani akiwa ni rais wa pili nchini Israel kuondokea wadhifa huo kufuatia fedheha.

Kwa mujibu wa maoni yaliyochapishwa na gazeti moja maarufu nchini humo Peres huenda akajizolea kura 50 huku Rivlin akipata kura 51 na mwisho akawa Avital amabaye huenda akapigiwa kura na wabunge 19 katika duru ya mwanzo.

Ili mgombea kuibuka mshindi katika kinyang’anyiri hicho itambidi kupata kura 61 na endapo hilo halitofanyika basi uchaguzi huo utaingia kwenye duru ya pili ambapo wagombea wawili wa mwanzo watapambana.

Na ikiwa duru ya pili itashindwa kumpata mshindi atakayejinyakulia kura 61 basi duru nyingin e ya tatu itafanyika na yule atakakuwa na kura nyingi zaidi ya mwenzake ndiye atakayekuwa rais mpya.

Peretz aliwahi kugombea nafasi hiyo miaka saba iliyopita na kutegemewa na wengi kwamba angeshinda uchaguzi huo lakini mambo yalikwenda vingine na ushindi huo ukanyakuliwa na Moshe Katsav wa chama cha Likud.

Peretz ni mwanasiasa anayependeza kwa jicho la kimataifa lakini ndani ya Israel amekuwa mtu wa kushindwa katika chaguzi kufuatia kushindwa kukiongoza kupata ushindi chama chake cha Labour kwenye chaguzi za bunge miaka ya 1977,1981,1984,1988,1996.

Vile vile ameshindwa mwaka 2000 katika uchaguzi war ais dhidi ya bwana Katsav na pia mwaka 2005 alikosa kupata ushindi wa kuongoza chama cha Labour ambapo baadaye aliamua kujitoa na kuingia kwenye chama kipya cha Kadima kilichoundwa na waziri mkuu wa zamani Ariel Sharon. Peretz amewahi kushikilia nyadhifa za waziri wa mambo ya nje na ulinzi nchini Israel.

A mezaliwa Poland mwaka 1923 na ana mke na watoto watatu na wajukuu kadhaa.

Shimon Peretz mwenye umri wa miaka 83 na mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel anapambana katika kinyanganyiro cha kuwania kiti cha Urais dhidi ya wagombea wengine wawili akiwemo spika wa zamani Reuven Rivlin wa chama cha mrengo wa kulia cha Likud na Colette Avital wa chama cha mrengo wa shoto kadirifu cha Labour.

Wabunge 120 watapiga kura kwa njia ya siri mchana wa leo kumchagua mrithi wa rais Moshe Katsav anayeandamwa na kashfa ya kumbaka mwanamke.

Kutoka na tuhuma hizo rais Katsav inambidi angatuke madarakani akiwa ni rais wa pili nchini Israel kuondokea wadhifa huo kufuatia fedheha.

Kwa mujibu wa maoni yaliyochapishwa na gazeti moja maarufu nchini humo Peres huenda akajizolea kura 50 huku Rivlin akipata kura 51 na mwisho akawa Avital amabaye huenda akapigiwa kura na wabunge 19 katika duru ya mwanzo.

Ili mgombea kuibuka mshindi katika kinyang’anyiri hicho itambidi kupata kura 61 na endapo hilo halitofanyika basi uchaguzi huo utaingia kwenye duru ya pili ambapo wagombea wawili wa mwanzo watapambana.

Na ikiwa duru ya pili itashindwa kumpata mshindi atakayejinyakulia kura 61 basi duru nyingin e ya tatu itafanyika na yule atakakuwa na kura nyingi zaidi ya mwenzake ndiye atakayekuwa rais mpya.

Peretz aliwahi kugombea nafasi hiyo miaka saba iliyopita na kutegemewa na wengi kwamba angeshinda uchaguzi huo lakini mambo yalikwenda vingine na ushindi huo ukanyakuliwa na Moshe Katsav wa chama cha Likud.

Peretz ni mwanasiasa anayependeza kwa jicho la kimataifa lakini ndani ya Israel amekuwa mtu wa kushindwa katika chaguzi kufuatia kushindwa kukiongoza kupata ushindi chama chake cha Labour kwenye chaguzi za bunge miaka ya 1977,1981,1984,1988,1996.

Vile vile ameshindwa mwaka 2000 katika uchaguzi war ais dhidi ya bwana Katsav na pia mwaka 2005 alikosa kupata ushindi wa kuongoza chama cha Labour ambapo baadaye aliamua kujitoa na kuingia kwenye chama kipya cha Kadima kilichoundwa na waziri mkuu wa zamani Ariel Sharon. Peretz amewahi kushikilia nyadhifa za waziri wa mambo ya nje na ulinzi nchini Israel.

Amezaliwa Poland mwaka 1923 na ana mke na watoto watatu na wajukuu kadhaa.