1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wachambuzi wasisitiza uwazi suala la chanjo, Tanzania

John Juma29 Januari 2021

Miito inazidi kutolewa kwa serikali ya Rais John Magufuli kubadili msimamo wake kuhusiana na janga la COVID-19. Baadhi ya viongozi wa taifa na wa mashirika ya kimataifa ikiwemo Shirika la Afya Duniani WHO wameitaka Tanzania kujiandaa kwa chanjo. Hata hivyo Magufuli ameshikilia kuwa nchi hiyo haina corona na kutilia mashaka ubora wa chanjo. Mwanaharakati Helen Kijo Bisimba alizungumzia hili.

https://p.dw.com/p/3oaSc