1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wafaransa 6 wagoma chakula

9 Desemba 2007

---

https://p.dw.com/p/CZKr

Raia 6 wa kifaransa waliowekwa kizuizini nchini Chad wameanza mgomo wa kukataa kula chakula.Wanadai hatima yao imesahauliwa.Wafanyikazi hao wa shirika la misaada ya kiutu Zoe’s Ark wanadai wana hisia serikali ya Ufaransa imewaacha mkono.

Wafaransa hao , wametuhumiwa kujaribu kuwakimbiza hadi watoto wadogo 100 kinyume na sharia kutoka Chad ili kulelewa nchini Ufaransa.

Shirika hilo wakati ule lilidai kwamba, wakidhani watoto hao walitoka Dafur, nchini Sudan- mkoa uliokumbwa na maafa ya vita.UM lakini uliarifu wengi wao wametoka vijiji vya nchini Chad.Tarehe ya kufunguliwa mashtaka wafaransa hao 6 bado haikuwekwa.