1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waislamu washerehekea Eid Ul Fitr, baada ya Ramadhani

Mohammed Khelef
10 Aprili 2024

Leo 10.04.2024 ni sikukuu ya kwanza ya Eid-ul-Fitr, baada ya kumalizika kwa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa waumini wa Kiislamu.

https://p.dw.com/p/4ebDl
Bangladesch Islam l Eid-ul-Fitr
Sherehe za Eid zimeanza rasmi ulimwenguni kwa waumini wa kiislamu baada ya kumalizika mfungo wa mwezi wa RamadhaniPicha: Ahmed Salahuddin/NurPhoto/picture alliance

Mamlaka nchini Saudi Arabia, taifa lenye misikiti miwili mitukufu kabisa kwa Waislamu, zilitangaza jioni ya jana kuwa waumini wa Kiislamu walitimiza siku 30 za kufunga na kwamba leo sala za iddi zitaswaliwa kote kwenye mamlaka hiyo.

Matangazo kama hayo yalisikika pia kutoka mamlaka za kidini za mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, Amerika, Arabuni, Ulaya na Asia.

Leo ni sikukuu ya Eid-ul-Fitr

Hapa nchini Ujerumani, Rais Frank-Walter Steinmeier ametuma salamu zake za Eid kwa Waislamu wa Ujerumani akiwapongeza kwa kukamilisha ibada ya mfungo wa Ramadhani, aliosema ni sehemu ya maisha ya jamii ya Kijerumani.

Ramadhani ni mojawapo ya nguzo tano za Uislamu, ambapo waumini wa dini hiyo hujizuwia kula, kunywa na mambo mengine yaliyokatazwa kwa mwezi mzima, kuanzia asubuhi hadi jioni kila siku.