1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wakongo kuhamishwa kuruhusu uchimbaji wa madini ya dhahabu

Josephat Nyiro Charo23 Julai 2010

Haijabainika wazi ni kiasi gani cha fedha kitakacholipwa Wakongo hao kama fidia wakati watakapohamishwa kutoka maeneo yao

https://p.dw.com/p/OTQx
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Joseph KabilaPicha: AP Photo

Watu 15 elfu watahamishwa makwao ili kurahisisha uchimbaji wa madini ya dhahabu na kampuni ya Uingereza na Afrika ya Kusini ya ANGLOGOLD kwenye vijiji kadhaa vya vimbo la Orientale, kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Kampuni hiyo imeahidi kuwajengea makaazi mapya na kuunda ajira. Mradi huo umezusha tofauti kubwa baina ya serikali na mashirika ya kiraia ya jimbo hilo ambayo yamehisi kwamba hatua ya kuhamishwa kwa raia bila hiari yao inakiuka haki za binadamu, huku wanaharakati wa kimazingira wakionyesha pia wasiwasi wao kuhusu hatua hiyo ya serikali na kampuni ya Anglogold. Taarifa kamili na mwandishi wetu Saleh Mwanamilongo

Mwandishi:Saleh Mwanamilongo

Mhariri:Josephat Charo