1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanajeshi wa umoja wa ulaya kupelekwa Bangui

29 Januari 2014

Baraza la usalama la umoja wa mataifa limependekeza kuwepo idadi ya wanajeshi zaidi ya elfu kumi katika Jamhuri ya afrika ya Kati kwa ajili ya kulinda amani.

https://p.dw.com/p/1AypL
Vikosi vya Umoja wa Ulaya kwenda Jamhuri ya Afrika ya Kati

Tayari kikosi cha umoja wa Ulaya kimepewa ruhusa na Umoja wa mataifa ya kwenda Jamhuri ya Afrika Kati ili kuwalinda raia.Kwenye azimio lililopitishwa kwa kauli moja na wanamemba 15 wa Baraza la Usalama la Umoja wa mataifa ni kwamba viongozi wa makundi yaliohusika na ukiukaji wa haki za binaadamu wataekewa vikwazo na Umoja huo.Taarifa kamili na mwandishi wetu Saleh Mwanamilongo . Kusikiliza taarifa hiyo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.

Mwandishi: Salehe Mwanamilongo

Mhariri: Mohamed Abdulrahman