1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanawaeka Korea Kusini wanaweza kuvuka miaka 90

22 Februari 2017

Wanawake nchini Korea Kusini wanakadiriwa kupiundukia umri wa miaka 90 kwa mujibu wa jarida moja la habari za kisayansi la lijulikanalo kama "The Lancet medical journal."

https://p.dw.com/p/2Y4tN
Nordkorea Textil Fabrik Industrie Näherinnen Schneiderinnen Frau
Picha: Getty Images

Wanawake nchini Korea Kusini watakuwa wa kwanza duniani kuwa na umri wa kuishi wa zaidi ya miongo tisa ikikadiriwa kuwa zaidi ya miaka 90. Korea ya Kusini si taifa pekee duniani ambalo wanawake wanaweza kupindukia wastani wa kuishi wa mika tisini, kwa mujibu wa jarida la kimataifa la masuala ya sayasni  The Lancet medical journal mataifa mengine ambayo wanawake wanaishi umri mkubwa unaokaribia sawa na huo ni Ufaransa na Marekani. Utafiti huo uliofanywa na chuo kimoja cha Uingereza na Shirika la Afya Duniani ulijikita katika umri wa kuishi katika mataifa 35 yenye kuonesha nuru ya uzalishaji vuiwandani. Aidha unaonesha kuiwa  watu watakuwa wanaishi miaka mingi kuliko ilivyo wakati huu ifikapo 2030 na vilevile unasema matokeo yake yataleta changamoto katika ulipaji wa mafao ya uzeeni na hata katika vituo vya kulelea wazee kwa kuwa watu wataishi kwa muda mrefu zaidi.

Mwandishi: Sudi Mnette
Mhariri: Saumu Mwasimba