1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wapiganaji 40 wa upinzani wauwawa Syria

Josephat Nyiro Charo25 Oktoba 2013

Wanajeshi wa serikali ya Syria leo wamewavamia waasi karibu na mji mkuu, Damascus, na kuwaua wapiganaji wapatao 40 wa upinzani. Mji wa kaskazini wa Safira, kusini mashariki mwa Aleppo, pia umeshambuliwa.

https://p.dw.com/p/1A6MD
This image made from amateur video released by Ugarit News, which has been authenticated based on its contents and other AP reporting, shows smoke rises in Damascus, Syria, Friday, June 21, 2013. The commander of Syria's rebels confirms they have received new weapons, giving his forces more power in battles against government troops and Hezbollah fighters from Lebanon. Gen. Salim Idris refused to say in an interview with Al-Jazeera TV Friday where the weapons came from. (AP Photo/Ugarit News via AP video)
Mapambano karibu na mji mkuu, DamascusPicha: picture-alliance/AP

Kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari uvamizi huo ulikuwa sehemu ya operesheni ya jeshi dhidi ya ngome za waasi zinazouzunguka mji huo, makao makuu ya utawala wa rais wa nchi hiyo, Bashar al Assad. Uvamizi huo karibu na Damascus umefanywa saa chache baada ya vikosi vya rais Assad kuuteka mji wa Hatitat al-Turkomen, kusini mwa mji huo, na hivyo kudhibiti barabara muhimu inayouunganisha mji huo mkuu na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Damascus.

Shirika la habari la serikali, SANA, limesema waasi 40 wameuwawa katika hujuma hiyo iliyotokea karibu na eneo la Otaiba, na kwamba shehena kubwa ya silaha imepatikana, yakiwemo makombora ya kuripua vifaru. Eneo hilo ni sehemu ya ukanda unaojulikana kama Ghouta Masharki, ambako kulifanyika shambulizi la silaha za sumu mwezi Agosti mwaka huu, ambapo mamia ya watu waliuwawa, wakiwemo wanawake na watoto.

ATTENTION EDITORS - VISUALS COVERAGE OF SCENES OF DEATH AND INJURY Syrian activists inspect the bodies of people they say were killed by nerve gas in the Ghouta region, in the Duma neighbourhood of Damascus August 21, 2013. Syrian activists said at least 213 people, including women and children, were killed on Wednesday in a nerve gas attack by President Bashar al-Assad's forces on rebel-held districts of the Ghouta region east of Damascus. REUTERS/Bassam Khabieh (SYRIA - Tags: CONFLICT POLITICS CIVIL UNREST) TEMPLATE OUT
Maiti za watu waliouwawa Ghouta na silaha za sumuPicha: Reuters

Afisa mmoja wa jeshi ambaye jina lake halikutajwa, ameiambia televisheni ya taifa ya Al-Ikhbariya kwamba wapiganaji wa kigeni ni miongoni mwa waliouwawa na shambulizi hilo limefanywa baada ya kupata taarifa za kijasusi. "Ilikuwa operesheni iliyofanikiwa. Tutaendelea kupata ushindi kutoka sehemu moja hadi nyengine," akaongeza kusema afisa huyo.

Mwanajeshi mwingine, ambaye hakutambulishwa kwa majina, amesema waasi ni wa kundi la Islam Brigade na Jabhat al Nusra au Al Nusra Front, lenye mafungamano na mtandao wa kigaidi wa al Qaeda. Shirika la haki za binaadamu la Syria lenye makao yake jijini London, Uingereza limesema wapiganaji wapatao 20 wameuwawa katika uvamizi huo, lakini halikutoa maelezo zaidi.

Wakati huo huo, helikopta za jeshi zimeushambulia mji wa kaskazini wa Safira, kusini mashariki mwa Aleppo. Kambi kubwa ya jeshi karibu na mji huo inaaminiwa ina kituo cha chini ya ardhi cha kinachotumiwa kutengeneza na kuhifadhi silaha za sumu. Shirika la madaktari wasio na mipaka limesema watu 130,000 wameukimbia mji wa Safria mwezi huu na kwamba mji huo umekuwa ukishambuliwa kwa mabomu tangu Oktoba 8. Taarifa ya shirika hilo imesema watu 76 wamekufa mjini humo.

Shambulizi la bomu

Katika tukio lengine la machafuko, shirika hilo limeripoti kuwa bomu lililokuwa limetegwa ndani ya motokaa limelipuka nje ya msikiti katika kijiji cha Suq Wadi Barada, na watu 40 ama wameuwawa au kujeruhiwa katika mlipuko huo. Hakuna taarifa za idadi kamili ya watu waliouwawa au kujeruhiwa katika mji huo, unaopatikana kaskazini magharibi mwa mji mkuu, Damascus.

Mkurugenzi wa shirika la haki za binaadamu la Syria, Rami Abdel Rahman, amesema miongoni mwa waliojeruhiwa ni watoto. Rahman aidha amesema ingawa mji huo uko mikononi mwa waasi, wanajeshi wanaomtii rais Assad wameuzingira. Televisheni ya taifa imeripoti juu ya shambulizi hilo, ikiwashutumu magaidi wenye mafungamano na al Qaeda. "Waasi wa kundi la Al Nusra Front wamelipua bomu karibu na msikiti wa Osama Bin Zeid katika kijiji cha Suq Wadi Barada katika mkoa wa Damascus. Taarifa za awali zinasema watu wameuwawa na wengine kujeruhiwa," ikatangaza televisheni hiyo.

Mapambano ya Wakurdi

Kuhusu mapambano kati ya Wakurdi na wapiganaji wa jihad shirika hilo limesema wapiganaji wa kikurdi wamezidi kusonga mbele katika mkoa wa Hassaekh wenye idadi kubwa ya Wakurdi. Wapiganaji hao waliingia mji wa Yaaroubiyeh leo na kukabiliana na makundi kadhaa ya jihad, yakiwemo Islamic State of Iraq na Al Nusra Front, yenye mafungamano na kundi la al Qaeda.

A Kurdish female fighter from the Popular Protection Units (YPG) carries a walkie-talkie as she stands near fellow fighters carrying their weapons and using binoculars in the Kurdish town of Ifrin, in Aleppo's countryside October 14, 2013. Kurds comprise around 10 percent of Syria's 23 million population. They are concentrated in Ifrin and other areas of the northwest, in parts of Damascus and in the northeastern oil producing area of Qamishli, where there has also been intense fighting between Kurds and al-Qaeda linked Islamic State of Iraq and the Levant fighters. Picture taken October 14, 2013. REUTERS/Roshak Ahmad (SYRIA - Tags: POLITICS CIVIL UNREST CONFLICT)
Wapiganaji wa Kikurdi nchini SyriaPicha: Reuters

Mji wa Yaaroubiyeh unaodhibitiwa na waasi uko katika kivuko kikuu cha mapakani kuingia nchini Iraq na kuuteka mji huo kutawapa wapiganaji wa Kikurdi njia rahisi ya kusafirishia bidhaa na mahitaji mengine kutoka eneo la Wakurid kaskazini mwa Iraq. Eneo hilo limeshuhudia mapiganao makali katika siku za nyuma na mapambano makali kati ya wapigaji wa Kikurdi na wapiganaji wa makundi ya jihad kaskazini mwa Syria yamesababisha vifo vya mamia ya watu katika miezi iliyopita.

Pia mwezi Machi mwaka huu wanaume waliokuwa wamejihami na bunduki waliwaua wanajeshi 51 wa Syria baada ya kuvuka na kuingia Iray kutoka Yaaroubiyeh. Wanajeshi hao walikuwa wameingia Iraq kutafuta hifadhi kufuatia mapambano na waasi upande wa Syria wa mpaka.

Mwandishi. Josephat Charo/APE/AFPE

Mhariri: Daniel Gakuba