1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

WASHINGTON: Olmert amewasili Marekani kwa mazungumzo na Bush

12 Novemba 2006
https://p.dw.com/p/CCtN

Waziri mkuu wa Israel,Ehud Olmert amewasili Washington nchini Marekani kwa mkutano wake wa pili pamoja na rais George W.Bush.Mkutano huo umepangwa kufanywa siku ya Jumatatu.Kufuatia matokeo ya hivi karibuni ya uchaguzi wa bunge nchini Marekani,Olmert amesema anataka kujiarifu juu ya siasa ya Washington kuhusu mgogoro wa Waisraeli na Wapalestina.Suala la Iran pia linatarajiwa kuchukua nafasi muhimu katika mazungumzo ya viongozi hao wawili.