1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

WASHINGTON: Robert Zoellick aidhinishwa rais wa Benki ya Dunia

26 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBoN

Bodi ya magavana wa Benki Kuu ya Dunia,kwa kauli moja imepiga kura kumuidhinisha Mmarekani,Robert Zoellick kama rais mpya wa wa benki hiyo.Paul Wolfowitz aliekuwa rais wa Benki Kuu ya Dunia, alikubali kuondoka madarakani mwezi uliopita,baada ya jopo maalum kuamua kuwa kiongozi huyo alikwenda kinyume na sheria za benki, alipompandisha cheo mpenzi wake na kumpatia nyongeza kubwa ya mshahara takriban miaka miwili iliyopita.