WASHINGTON: Wanachama wa Mafia waliajiriwa kumuua Rais Castro
27 Juni 2007Matangazo
Shirika la upelelezi la Marekani-CIA,liliajiri wanachama wa Mafia,kujaribu kumuua Rais wa Cuba Fidel Castro.Hilo ni miongoni mwa yale yaliyofichuliwa na hati zilizowekwa bayana,kwenye tovuti ya CIA katika mtandao wa Internet.Hati hizo vile vile zinaeleza kwa umbali gani shirika hilo lilimpeleleza adui wake wa enzi ya Vita Baridi,Soviet Union ya zamani pamoja na hata waandishi wa habari na raia wa Kimarekani waliopinga vita vya Vietnam.