1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

WASHINGTON: Wanajeshi wa Marekani kufikishwa mahakamani

20 Oktoba 2007
https://p.dw.com/p/C7EN

Wanajeshi 2 wa Marekani watafikishwa mbele ya mahakama ya kijeshi kwa mashtaka yanayohusika na mauaji ya raia wa Kiiraki katika mji wa Haditha nchini Irak.Inatuhumiwa kuwa Novemba mwaka 2005, wanajeshi wa Kimarekani waliwaua Wairaki 24 kulipiza kisasi kifo cha mwanajeshi mwenzao mjini Haditha.Miongoni mwa Wairaki waliouawa,10 walikuwa wanawake na watoto.