1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

WASHINGTON:Bush ataka fedha zaidi kwa ajili ya vita vya nchini Irak

6 Februari 2007
https://p.dw.com/p/CCUe

Rais G.Bush amewasilisha ombi la dola bilioni mia saba kwa ajili ya matumizi ya kijeshi ikiwa ni sehemu ya bajeti ya dola trilioni 2 nukta tisa anayotaka ipitishwe na bunge la nchi yake.

Sehemu kubwa ya dola hizo bilioni mia saba itatumika kwa ajili ya vita vya nchini Irak na Afghanistan.