1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

WASHINGTON:Rais Bush hatojifungamanisha na azimio la Irak

16 Februari 2007
https://p.dw.com/p/CCRZ

Rais George W.Bush wa Marekani amesema hatojifungamanisha na azimio litakalopitishwa na bunge kuhusu Irak,isipokuwa mswada wa azimio unaohusika na ombi la kuongeza pesa kwa ajili ya vikosi vya Marekani nchini Irak.Leo Baraza la Wawakilishi la Marekani linapiga kura na kesho Jumamosi,Seneti pia itapiga kura kuhusu azimio hilo ikiwa Marekani ipeleke wanajeshi 21,500 wengine nchini Irak.