1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 14 waungua hadi kufa huko Naivasha Kenya

28 Januari 2008
https://p.dw.com/p/CyX7

Watu takriban 14 waliungua hadi kufa hapo jana wakati walipokuwa wakijificha kutokana na machafuko ndani ya nyumba moja mjini Niavasha magharibi mwa Kenya.

Watu wengine tisa waliuwawa hapo kabla wakati wa mapambano makali kati ya magenge ya vijana kutoka maeneo ya madongo poromoka mjini humo.

Idadi ya watu waliouwawa magharibi mwa mkoa wa bonde la ufa imefikia 130 tangu Alhamisi wiki iliyopita.

Mauji yanayoendelea nchini Kenya yanadumaza juhudi za katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa Kofi Annan kujaribu kuutanzua mzozo wa kisiasa nchini Kenya uliosababishwa na matokeo ya uchaguzi wa mwaka jana.

Akiwa katika siku yake ya sita ya ziara yake nchini humo Kofi Annan jana alikutana na kiongozi wa upinzani Raila Odinga ambaye amelaani vikali mauaji yanayoendelea huko Naivasha.

Odinga amedai makundi ya wahalifu yanayolindwa na polisi yanawaua watu bila kujali.