1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 66 wauwawa nchini Syria

30 Januari 2012

Hali imeendelea kuwa mbaya nchini Syria ambapo watu 66 wameuwa katika mapigano makali nchini humo, huku serikali ya Ujerumani ikihimiza jumuiya ya kimataifa kufanya jitihada za haraka katika katika kudhibiti mauwaji hayo

https://p.dw.com/p/13skl
Syrian army defectors stand guard in the Deir Baghlaba area in Homs province, central Syria, on Friday, Jan. 27, 2012. Armed forces loyal to President Bashar Assad barraged residential buildings with mortars and machine-gun fire, killing at least 30 people, including a family of women and children during a day of sectarian killings and kidnappings in the besieged Syrian city of Homs, activists said Friday. (Foto:AP/dapd)
Wanajeshi waasiPicha: dapd

Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Ujerumani Guido Westerwelle jana ameanza ziara yake huko Mashariki ya Kati. Kituo cha kwanza katika ziara yake hiyo ya siku tano kilikuwa Amman, ambapo alielezea wito wa Ujerumani wa kutaka jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua za pamoja kukomesha machafuko nchini Syria.

Ujerumani ni miongoni mwa nchi wanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambao waliwasilisha rasimu ya maazimo yao kuhusu Syria ijumaa. Urusi, yenye kura ya turufu, imesema haitaunga mkono rasimu ya hali yake sasa.

Berlin/ Aussenminister Guido Westerwelle (FDP) gibt am Sonntag (29.01.12) in Amman, der Hauptstadt des Haschemitischen Koenigreichs Jordanien, eine Pressekonferenz. Westerwelle ist am Sonntag zu einer mehrtaegigen Nahost-Reise aufgebrochen. Ziel des Besuches ist, Bewegung in den festgefahrenen Friedensprozess zwischen Israelis und Palaestinensern zu bringen. (zu dapd-Text) Foto: Steffi Loos/dapd
Guido Westerwelle akiwa JordanPicha: dapd

Baada ya mkutano wake na waziri mwenziwe wa mambo ya nje wa Jordan, Westerwelle alitoa wito pia kwa Wapalestina na Waisreal kurejea katika meza ya mazungumzo. Waziri huyo wa mambo ya nje wa Ujerumani anatarajiwa kwenda Misri, kabla kutembelea pia himaya za Palestina na Isreal.

Katika hatua nyingine nchini Syria vikosi vya Rais Bashar al-Assad vimefanya mashambulizi makubwa katika vitongoji vinavyodhibitiwa na waasi mjini Damascus. Makundi ya haki za binadamu yanasema watu 66 wameuwawa wakiwemo raia 26.