Mitandao ya kijamii sio tu ni njia ya kuwasiliana na ama hata ya kujitangaza kibiashara, bali pia ni njia ya kuwasaidia wenye uhitaji. Hilo ndilo alilokumbana nalo Mohammed Khelef wakati akiwa visiwani Zanzibar, ambapo vijana wameunda kundi kwenye mtandao wa kijamii wa WhatsApp linalojihusisha na kuwapatia misaada watu wenye matatizo na wasiokuwa na wa kuwasaidia.