1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Weah kuchuana na Boakai duru ya pili ya uchaguzi

Caro Robi
16 Oktoba 2017

Tume ya uchaguzi nchini Liberia imetangaza kuwa aliyekuwa mwanasoka maarufu wa kimataifa George Weah na makamu wa Rais wa Liberia Joseph Boakai Watachuana katika duru ya pili ya uchaguzi wa rais.

https://p.dw.com/p/2ltTM
Fussball WM 2010  Qualifikationsgruppen - Auslosung Georg Weah
Picha: picture-alliance/dpa/Pressefoto ULMER/M. Ulmer

Tume ya uchaguzi nchini Liberia imetangaza kuwa aliyekuwa mwanasoka maarufu wa kimataifa George Weah na makamu wa Rais wa Liberia Joseph Boakai Watachuana katika duru ya pili ya uchaguzi wa rais inayotarajiwa tarehe 7 Novemba. Weah alipata asilimia 39 ya kura huku Boakai akipata asilimia 29.1 katika duru ya kwana ya uchaguzi uliofanyika Jumanne wiki iliyopita, hivyo hakuna mgombea aliyepata zaidi ya asilimia 50 ya kura ili kuepusha duru ya pili ya uchaguzi.

Atakayeshinda duru ijayo atamrithi Rais Ellen Johnson Sirleaf, mwanamke wa kwanza barani Afrika kuwa Rais anayesataafu baada ya kuwa madarakani kwa miaka 12. Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Jerome Korkoy amesema idadi ya wapiga kura iliyojitokeza kushiriki katika uchaguzi ilikuwa ni asilimi 74. Wapiga kura wana chaguo kati ya Boakai ambaye amehudumu katika nyadhifa mbali mbali serikalini kwa zaidi ya miongo mitatu au Weah ambaye ni maarufu mno licha ya kutokuwa na uzoefu  katika ulingo wa kisiasa.