1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Westerwelle ziarani India

Aboubakary Jumaa Liongo19 Oktoba 2010

Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani Guido Westerwelle yuko India katika ziara yake ya kwanza nchini humo tangu kuchukua wadhifa huo mwaka mmoja uliopita.

https://p.dw.com/p/PhuY
Waziri wa Nje wa India S.M. Krishna, kushoto, na mgeni wake Guido Westerwelle wa UjerumaniPicha: AP

Ziara  ya   Westerwelle  katika  nchi  hii  yenye  demokrasia  kongwe  kabisa duniani, pamoja  na  idadi  kubwa  ya  wakaazi  ni  mambo  yanayomvutia sana.

Waziri  anatambua  hamasa  walioyonayo  raia  wa  nchi  hii  katika kujishughulisha,  pamoja  na  ukuaji  wa  uchumi, na  pia  katika  hali mnyumbuliko  ya  nchi  hiyo.  Hayo  yote  anayatambua.

Ni  lazima  mtu  , anapoangalia  dunia , kutambua , ni  kiasi  gani  nchi zinavyojaribu kujitokeza  kwa  kasi  na   zinavyotaka  kupanda  juu,  hili linapaswa  kutambuliwa.

Westerwelle  hana  maneno  zaidi  ya  kuisifu  India  na  juhudi  zake  za kujiimarisha  duniani. 

Baada  ya  mazungumzo  na   waziri  mwenzake   pamoja  na  waziri  mkuu, ameitaka  India  kuchukua  jukumu  la  mbele  katika  ulinzi  wa  mazingira pamoja  na  kushughulikia   mizozo  ya  kimkoa, akitambua  wazi  kuwa , kutokana  na  maslahi  yake  ya  kiuchumi   ulinzi  wa  mazingira  kwa  India  ni suala  gumu.

India  ni  sehemu  muhimu   ya  nguvu  za  demokrasia  inayoleta  uthabiti katika  eneo  la  Asia, na  ndio  sababu  tunahitaji  kuimarisha  ushirika  na India.

Maadili  haya  ya  pamoja  ndio  msingi  wa  hatua  za  kufanyakazi  kwa pamoja  kati  ya  India  na  Ujerumani, pamoja  na  mkakati  wa  ushirika  wetu.

Mkakati wa  ushirika   na  India  unaweza  kujaribiwa  katika  baraza  la usalama  la  umoja  wa  mataifa, kwa  kuwa  nchi  zote  mbili ni  wanachama ambao  si  wa  kudumu  wa  baraza  la  usalama  la   umoja  huo, na  nchi zote  zinataka  mageuzi   katika   umoja  wa  mataifa.

Kwa  hilo  hata  hivyo  waziri   Westerwelle  anachukua  tahadhari  sana. Amesema  kuwa  suala  la  mageuzi  katika  umoja  wa  mataifa  si  suala  la nchi  gani  ina  nguvu  sana  katika  baraza  la  usalama  ama  ipi  ni  dhaifu, suala  ni  ulazima  wa  kuufanyia  mageuzi  umoja   wa  mataifa  ili  kuufanya kuwa  na  nguvu  zaidi.

Pia  waziri  Westerwelle  amesema  baada  ya  mazungumzo  na  waziri mkuu  Manmohan Singh  na  waziri  wa  mambo  ya  kigeni  SM Krishna   mjini New Delhi  kuwa  itakuwa  ni  hatua  kubwa  mbele  iwapo  India   itatia  saini mkataba  unaopiga  marufuku   majaribio  ya  silaha  za  kinuklia.

India  inapinga  hatua  kama  hiyo, ikisema  kuwa   makubaliano  kama  hayo yanaugawa  ulimwengu  baina  ya   mataifa   yenye  silaha  za  kinuklia  na yale  ambayo  hayana.

 Kuhusu  suala  la  Iran  waziri  Guido  amesema  kuwa  kuna  hali  ya kukubaliana, kwamba  hakuna  mtu  katika   jamii  ya  kimataifa  ambaye anaona  kuna  maslahi  kwa  Iran  kutumia  tekolojia  ya  kinuklia  iliyonayo kwa  njia  mbadala   ya  kuunda  silaha , mtazamo  huu  upo  kwa  serikali zetu  zote  mbili.

Ziara  ya  waziri  Westerwelle  inamalizika  leo Jumanne.

Mwandishi : Kostolnik , Barbara / ZR / Sekione  Kitojo

Mhariri :  Aboubakary Liongo.