Nchini Tanzania hatimaye wabunge wateule wa viti maalum wa chama kikuu cha upinzani, CHADEMA wameapishwa hii leo katika viwanja vya Bunge mjini Dodoma// NATO, EU wamwalika Biden kujenga upya uhusiano na Marekani// Pande zinazozozana nchini Ethiopia zinatupiana maneno makali ambayo Umoja wa Mataifa unahofia yanaweza kuchochea zaidi ukiukaji wa haki za binadamu na wananchi kuzidi kuumia.