Kiongozi wa chama kikuu cha upinzani kwa sasa nchini Uganda Robert Kyagulanyi amekariri kuwa harakati zake za kumng’oa rais Museveni zinaendelea// Rais wa Afrika Kusini na mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Cyril Ramaphosa ameyatolea wito mataifa tajiri kutohodhi dozi za ziada za chanjo ya Covid-19// Mawaziri wa mambo ya nje wa Urusi na Iran wametoa wito wa kuokolewa kwa mkataba wa nyuklia wa Iran.