1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Amirijeshi abadilishwa Iran

2 Septemba 2007
https://p.dw.com/p/CBTU

TEHERAN:

Kiongozi mkuu wa kidini nchini Iran,Ayatollah Ali Khamenei, amembadilisha kamanda wa Jeshi la kimapinduzi humo nchini.Kituo cha TV cha Iran kimeripoti kwamba amirijeshi-mkuu wa zamani Yahya Rahim Safavi nafasi yake inachukuliwa sasa na Mohammad Ali Jaafari.

Hakuna sababu kwanini mabadiliko hayo yanafanyika.

Jeshi la walinzi wa mapinduzi liliundwa muda mfupi baada ya mapinduzi ya kiislamu ya 1979.