1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ATHENS: Misitu na nyumba zateketezwa na moto

28 Julai 2007
https://p.dw.com/p/CBeX

Wazima moto nchini Ugiriki na Italia wanaendelea kupambana na moto uliosambaa misituni.Maafisa kusini mwa Italia,wametangaza hali ya maafa baada ya misitu kuendelea kushika moto tangu siku tano, kwa mfululizo.Zaidi ya wazima moto 200 wakisaidiwa na wanajeshi na helikopta mbili wanahangaika kuzima moto ulioteketeza kiasi ya nyumba 100 katika eneo la kusini la Peloponnes. Bulgaria na Croatia pia zimeripoti juu ya misitu iliyoshika moto.