1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ATHENS: Ubalozi wa Marekani mjini Athens washambuliwa

12 Januari 2007
https://p.dw.com/p/CCbN
Mwanamke akienda sokoni Afrika Kusini
Mwanamke akienda sokoni Afrika KusiniPicha: AP

Mlipuko umetokea kwenye ubalozi wa Marekani mjini Athens Ugiriki kufuatia shambulio la roketi. Afisa wa polisi mjini humo amekitaja kitendo hicho kuwa cha kigaidi. Wizara ya mambo ya ndani ya Marekani imetangaza mjini Washinton kwamba hakuna aliyejeruhiwa katika hujuma hiyo.

Magari kadhaa ya polisi yameuzunguka ubalozi wa Marekani mjini Athens na maofisa wa polisi wamezifunga barabara zote zinazoelekea eneo hilo, ikiwa ni pamoja na bustani lililo mbele ya ubalozi huo.

Vikosi vya usalama na vya kupambana na ugaidi vya Ugiriki vinalichunguza eneo la tukio. Kundi la waasi linalolitishia usalama nchini Ugiriki, liitwalo Novemba 17, ambalo zamani liliwaua wanadiplomasia wa Marekani na wa mataifa mengine ya kigeni, lilivunjwa mnamo mwaka wa 2002.