1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

AU kuimarisha juhudi za amani ya Libya

10 Februari 2020

Umoja wa Afrika umeapa kuongeza nguvu katika juhudi za umoja wa mataifa kwa kutafuta suluhiso katika mzozo wa Libya, Mkuu wa baraza la usalama la AU Smail Chergui amesema wakati umoja huo ukikutana Addis Ababa, Ethiopia

https://p.dw.com/p/3XZ0G
Äthiopien AU-Gipfel in Addis Abeba | Cyrial Ramaphosa übernimmt Vorsitz von Abdel Fattah al-Sisi
Picha: picture-alliance/AP Photo

Katika mkutano huo wa siku mbili  chini ya kauli mbiu ''Kukomesha vita barani Afrika'' viongozi na wawakilishi kutoka kote Afrika wamezitaka pande zinazopigana nchini Libya  kufikia makubaliano ya kuweka chini silaha.

Hata hivyo Umoja wa  Afrika  umelalamika kwa  kuachwa nje  katika kusaka suluhisho  katika  mzozo huo ambao umedumu kwa zaidi ya miaka saba sasa,  AU inasema michakato yote ya  UN, imeendelezwa hasa na mataifa ya Ulaya pekee. Lakini Chergui alieleza kuwa umoja huo utaunga mkono makubaliano ya kuweka chini silaha ya pande hasimu.

''Kwa wakati huu, ni Umoja wa Mataifa (UN) unaotuhitaji sisi (AU), mashirika haya lazima yashirikiane kwa lengo hilo "amani ya Libya" Amesema Smail Chergui, mkuu wa baraza la usalama la AU; wakati akizungumza na wanahabari leo Jumatatu mjini Addis Ababa, kwenye mkutano wa kilele wa AU wa awamu ya 33.

Libya imegubikwa na mapigano ya makundi kadhaa ya kujihami tangu jumuiya ya kujihami ya NATO  kumuondoa  madarakani  rais wa kimla Moamer Gadhafi, mnamo mwaka 2011.

Wakati huo Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa Antonio Guterres amesema anafahamu masikitiko ya Umoja wa Afrika kwa kutohusishwa katika masuala ya mzozo wa Libya.

Cyril Ramaphosa, rais wa Afrika kusini ambaye anachukua hatamu ya uenyeiti wa umoja huo amesema atazingatia  masuala ya kurejesha amani nchini Libya.

Nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika imekumbwa na mapigano kati ya mbabe wa kivita Khalifa Haftar anaedhibiti maeneo ya mashariki wa nchi hiyo na serikali ya Tripoli inayoungwa mkono na Umoja wa mataifa.

Majadiliano ya kusitisha mapigano kati ya pande hasimu yalikamilika jumamosi bila kufua dafu ya kusainiwa kwa makubaliano. Umoja wa mataifa umependekeza Februari 18 kama siku kufanyika tena kwa mazungmzo hayo.