1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

AUGUSTA: Jamaa na marafiki wamuaga James Brown

31 Desemba 2006
https://p.dw.com/p/CCei

Jamaa, marafiki, mashabiki na viongozi wa haki za raia wamekusanyika kutoa heshima zao za mwisho kwa mwanamuziki wa miondoko ya soul, James Brown, wiki moja baada ya kifo chake.

Maelfu ya watu wamesafiri kwenda mjini Augusta alikozaliwa mwanamuziki huyo kutoa heshima zao katika sherehe ya hadhara kwenye ukumbi wa James Brown mjini humo. James Brown alifariki dunia siku ya kulalia sikukuu ya Krimasi huko Atlanta akiwa na umri wa miaka 73.