1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Bayern Munich kuwavaa Lazio

22 Februari 2021

Mechi za Ligi ya Vilabu Bingwa barani Ulaya zitakuwa zinarindima kwa mara nyengine tena Jumanne ambapo mabingwa Bayern Munich watacheza na Lazio ya Italia katika harakati za kupigania kutetea ubingwa wao hapo kesho.

https://p.dw.com/p/3phyl
Fußball: Bundesliga 2021 I Eintracht Frankfurt - Bayern München
Picha: Daniel Roland/POOL/AFP

Jumatano Real Madrid ambayo inashikilia rekodi ya kulishinda taji hilo watakuwa wanasafiri kuelekea Italia kucheza na Atalanta na kutokana na masharti ya kuzuia kusambaa kwa virusi vya corona, Atletico Madrid watacheza mechi yao dhidi ya Chelsea huko Bucharest huku Manchester City wakipambana na Borussia Mönchengladbach huko Budapest.