1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Bayern Munich yaisubiri Real Madrid

Sekione Kitojo
23 Aprili 2018

Bayern yaisubiri  kwa  hamu  Real Madrid  katika  mtanange wa Champions League  wa kulipiza  kisasi.

https://p.dw.com/p/2wWa7
Deutschland FC bayern München
Kikosi hatari cha Bayern MunichPicha: imago/kolbert-press

Champions League  inarejea  uwanjani  tena  kesho  na  keshokutwa Jumatano katika  awamu  ya  nusu  fainali, ambapo  klabu  kutoka ligi  nne  kubwa  za  Ulaya  zinawakilishwa. Kwa  mara  ya  kwanza tangu  mwaka 1981, timu  kutoka Uhispania , Real Madrid  England Liverpool, Italia  Roma  na  Ujerumani  Bayern Munich zinakuwa  timu nne  za  mwisho  katika  kinyang'anyiro  hicho cha  juu  cha  vilabu barani  Ulaya.

Fußball Manchester City v Liverpool - Mohamed Salah
Mo Salah wa LiverpoolPicha: picture-alliance/Newscom/D. Klein

Roma  inasafiri  kwenda  mjini  Liverpool   kwa  mkondo  wa  kwanza wa  nusu  fainali  ya  Champions League, wakitarajia  kupata matokeo  mazuri  ambayo  yalianzia  katika  kuitupilia  mbali Barcelona.  Kocha  wa  Roma  Eusebio Di Francesco  anakichukua kikosi  chake  kwenda  Liverpool  kesho  Jumanne  katika  mchezo huo  wa  kwanza.

Champions-League Manchester City vs Liverpool
Kocha wa Liverpool Jurgen KloppPicha: Getty Images/L. Griffiths

Di Francesco , aliyechukua  nafasio  ya  Luciano Spalletti  Juni mwaka  jana, alikuwa  kijana  mwaka  1984 wakati  Liverpool ilipoigaragara  Roma  nyumbani  katika  fainali ya  kombe  la  Ulaya, kama  lililvyokuwa  linafahamika  wakati  huo.

Liverpool ilinyakua  taji lake  la  nne kati ya mataji  matano  ya  bara  la  Ulaya  kwa kupigiana  penalti  baada  ya  kutoka  sare  kwa  bao 1-1 katika uwanja  wa  Stadio Olimpico.

Miaka 17  baadaye  Di Francesco alikuwa  katika  benchi  la  Giallorossi  akiwa  mchezaji  wa  kiungo akiwaangalia  Liverpool wakishinda  kwa  mara  nyingine  tena  kwa jumla ya  mabao 2-1, katika  timu 16 zilizobakia katika  kombe  la UEFA  mwaka  2001.

Champions League 2013 FC Bayern München - Real Madrid
Picha: picture-alliance/dpa/H. Rudel

Lakini  siku  ya  Jumatano  kutakuwa  na  patashika  nyingine  ya nusu  fainali, wakati  bayern  Munich  ikicheza  nyumbani  katika mchezo  wa  mkondo  wa  kwanza , ina malengo  ya  kulipiza  kisasi cha  kufungwa  msimu  uliopita  na  Real Madrid  katika  michezo yote  miwili  katika  robo  fainali.

Bayern Munich imekuwa  na matatizo  na  timu  za  Uhispania hivi  karibuni  na  kuondolewa mashindanoni  katika  misimu  minne  mfululizo dhidi  ya  timu  za Uhispania. Bayern  iliondolewa  mashindanoni  na  Real mwaka 2014, Atletico  Madrid  mwaka 2015 na  barcelona 2016. Mwaka jana  Real  iliiondoa  Bayern  katika  robo  fainali. Real Madrid inawania  kulibeba kombe  hilo  kwa  mara  ya  tatu  mfululizo.

 

Mwandishi: Sekione  Kitojo / dpae / afpe / rtre

Mhariri: Yusuf , Saumu