1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nani zaidi, Bayern au Leverkusen?

Deo Kaji Makomba
2 Julai 2020

Bayern Munich Jumamosi (04.07.2020) wanatarajia kushuka uwanjani kukabiliana uso kwa uso na timu ya Bayer Leverkusen katika mchezo wa fainali wa kombe la shirikisho, DFB Pokal.

https://p.dw.com/p/3ei1J
Fußball Bundesliga Übergabe Meisterschale FC Bayern München
Mabingwa mara nane wa Bundesliga, Bayern MunichPicha: Reuters/K. Pfaffenbach

 Mabingwa mara nane mfululizo wa ligi ya soka nchini Ujerumani Bundesliga, Bayern Munich Jumamosi (04.07.2020) wanatarajia kushuka uwanjani kukabiliana uso kwa uso na timu ya Bayer Leverkusen katika mchezo wa fainali wa kombe la shirikisho, DFB Pokal.

Bayern ambao walifanikiwa kulitwaa taji la Bundesliga katika msimu uliomalizika wa Bundesliga, msimu uliobadilishwa na mlipuko wa virusi vya Corona, kwa sasa inatamani tena kuongeza taji lengine.

Kinyume chake timu ya Leverkusen haijaonja mafanikio tangu mwaka 1993 licha ya kunyemelea kwa karibu kulitwaa taji la Bundesliga takribani mara nane, kombe la DFB Pokal pamoja na ligi ya mabingwa barani Ulaya.

 

Fussball 1. Bundesliga 19.Spieltag l Bayer 04 Leverkusen vs Fortuna Düsseldorf l Jubel
Wachezaji wa Bayer Leverkusen wakifurahia moja ya ushindi katika mechi ya BundesligaPicha: picture alliance/AP Photo/M. Meissner

"Tutaendelea kuwa na njaa," alisema mchezaji wa Bayern, Joshua Kimmich, baada ya kufanikiwa kulitwaa taji la Bundesliga.

Wakati Bayern ikisonga mbele, ni ngumu kuacha lakini mshangao sio haiwezekani. Walipoteza fainali ya kombe la shirikisho mwaka 2018 kwa Eintracht Frankfurt lakini hiyo ni hatua yao ya pekee katika muonekano wao wa tano wa mwisho katika mechi ya kuonyesha.

Matumaini ya kurudia tena kushinda mataji matatu kama mwaka 2013 bado yapo huku ligi ya mabingwa wa Ulaya ikitarajiwa kurejea tena dimbani mwezi Agosti mwaka huu. Bayern wanakaribia kufuzu kwa robo fainali, baada ya kushinda mechi yao ya ugenini dhidi ya Chelsea kwa idadi ya kutosha ya magoli.

Msimu huu ni wa kusisimua ikizingatiwa jinsi timu ya Bayern Munich ilivyopambana chini ya kocha wa zamani, Niko Kovac, mapema katika msimu huu. Lakini ujio wa kocha Hansi Flick mwezi Novemba 2019 uliashiria mageuzi katika mkondo wa mambo na Bayern sasa hawajashindwa katika mechi 25 za mashindano zilizopita, ikishinda mechi 24.

"Ilikuwa ngumu lakini mwishowe ilikuwa na nguvu sana," alisema mshambuliaji Robert Lewandowski, ambaye aliibuka mfungaji bora kwenye Bundesliga akipachika magoli 34.

Bayern wako katika mfululizo wa ushindi wa mechi 16 ikijumuisha kipigo cha magoli 4-2 kwa Leverkusen licha ya kuwapa wenyeji goli kwanza.

Lakini Leverkusen iliishinda Bayern mapema ikiwa chini ya kocha Flick, hata kama bahati ilikuwa upande wao katika ushindi huo wa mabao 2-1

Chanzo/dpa