1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BEIJING: Mazungumzo ya mataifa sita yashindwa kufua dafu

22 Desemba 2006
https://p.dw.com/p/CCh8

Mazungumzo ya mataifa sita kuhusu mpango wa nyuklia wa Korea Kaskazini yamemalizika leo mjini Beijing China pasipo makubaliano kufikiwa. Shirika la habari la Korea Kusini limeripoti kwamba hakuna tarehe nyengine ya mazungumzo iliyopangwa.

China iliyoyaandaa mazungumzo hayo imesema lengo kubwa lilikuwa kulifanya eneo la Korea kuwa huru kutokana na silaha hizo. Mazungumzo hayo yalianza Jumatatu wiki hii baada ya kukwama kwa miezi 13.

Serikali ya Pyongyang imeitaka Marekani iondoe vikwazo vyake vya kifedha dhidi yake pamoja na kufunguliwa kwa akaunti za benki zilizofungiwa. Korea Kaskazini ilifanya majaribio ya zana zake za kinyuklia mnamo Oktoba 9 mwaka huu.