1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BEIRUT: Wanamgambo washambuliwa kambi ya Nahr al-Bared

9 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBtI

Nchini Lebanon,vikosi vya serikali vimeshambulia tena vituo vya wanamgambo wa Fatah al-Islam waliojificha katika kambi ya wakimbizi wa Kipalestina ya Nahr-al-Bared.Wanamgambo hao,tangu majuma kadhaa sasa,wanajificha katika kambi hiyo,kaskazini mwa Lebanon.Mashahidi wamesema, kambi hiyo imeshambuliwa na kama maguruneti 20 yaliosababisha moto.