1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BEIRUT : Waziri wa viwanda auwawa

21 Novemba 2006
https://p.dw.com/p/CCqb

Waziri wa viwanda nchini Lebanon Pierre Gemayel ameuwawa na watu wenye silaha karibu na Beirut leo hii.

Duru za usalama zimesema watu hao wenye silaha waliushambulia kwa risasi msafara wake wakati ukipita kwenye kitongoji cha Wakristo cha Sin el Fil.

Gemayel alikimbizwa hospitali ambapo baadae alikufa kutokana na majeraha ya risasi.