1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BRAZAVILLE: Kura zimeanza kuhesabiwa

25 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBoX

Kura zimeanza kuhesabiwa baaada ya duru ya kwanza ya uchaguzi wa bunge nchini Jamuhuri ya Kongo Brazaville, lakini habari zinasema kuwa idadi ya wapiga kura ilikuwa ndogo na tume ya uchaguzi imesema kuwa makosa yamefanyika.

Matokeo rasmi yanatarajiwa kufahamika baada ya wiki moja.

Vyama 40 vya kisiasa vimesusia uchaguzi huo kwa madai kwamba una lengo la kuimarisha utawala wa rais Denis Sassou-Nguesso ambae ameishakaa madarakani kwa muda wa miaka 23.