1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

CANBERA: Howard aahidi msaada zaidi kwa Irak

19 Februari 2007
https://p.dw.com/p/CCQn

Waziri mkuu wa Australia, John Howard, amesema nchi yake huenda ikaongeza msaada wake nchini Irak. Hata hivyo, Howard hakusema ikiwa atapeleka wanajeshi zaidi kwenda Irak.

Idadi ya wanajeshi nchini Irak na Afghanistan inatarajiwa kuwa mada muhimu wakati wa mazungumzo yake na makamu wa rais wa Marekani, Dick Cheney, atakayeitembelea Australia wiki hii.

Howard amesema walimu wa jeshi zaidi huenda wakapelekwa Irak, ambako wanajeshi 1,400 wa Ausatralia wanahudumu.