Colin Powell amuunga mkono Obama
19 Oktoba 2008Washington:
Waziri wa zamani wa mambo ya nchi za nje wa Marekani katika utawala wa Rais wa sasa George W.Bush, Colin Powell ametangaza kumuunga mkono mgombea wa Wademocrats katika uchaguzi ujao wa rais nchini humo Barack Obama. Colin Powell alisema wote wawili Obama na mpinzani wake mgombea wa Raepublican John MacCain wanasifa za kuweza kuwa Amiri Jeshi mkuu, lakini Obama anaweza kuyashughulikia vizuri zaidi masuala ya uchumi na kuboresha sifa na msimamo wa Marekani duniani. Bw Powell alielezea kusikitishwa kwake na matamshi anayotumia Bw McCain katika kampeni yake pamoja na uteuzi wake wa Gavana wa Alaska Sarah Palin kuwa mgombea mwenza wa Warepublican. Alisema haamini Palin anauwezo wa kushika wadhifa wa Urais ikilazimika.Uchaguzi wa Rais nchini Marekani utafanyika tarehe 4 mwezi ujao wa Novemba