1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

COLOMBO: Watu 40 wauwawa katika mapigano

21 Oktoba 2006
https://p.dw.com/p/CD0a

Watu takriban 40 wameuwawa katika mapigano ya hivi punde nchini Sri Lanka. Boti za jeshi la wanamaji ziliziharibu boti saba za waasi wa Tamil Tigers katika mapigano ya baharini hapo jana na kuwaua waasi wasiopungua 35.

Waasi wengine sita wameuwawa katika mapigano mengine yaliyozuka leo asubuhi kwenye ngome ya waasi wa Tamil Tigers huko Jaffna kaskazini mwa nchi hiyo.

Sri Lanka imekabiliwa na ongezeko kubwa la machafuko katika miezi michache iliyopita, hivyo kuzusha wasiwasi ikiwa kweli mazungumzo ya kutafuta amani kati ya serikali na waasi wa Tamil Tigers yaliyopangwa kufanyika mjini Geneva, Uswisii kati ya tarehe 28 na 29 mwezi huu, yatafaulu.