Dakar. Rais Wade athibitishwa mshindi.
12 Machi 2007Matangazo
Baraza la katiba nchini Senegal limemtangaza rasmi rais Abdoulaye Wade kuwa mshindi wa uchaguzi uliofanyika wiki mbili zilizopita.
Baraza hilo ambalo ndio chombo cha juu kabisa nchini humo kinachotoa maamuzi juu ya masuala ya uchaguzi limesema kuwa Wade ameshinda uchaguzi huo kwa asilimia 55.9 ya kura zilizopigwa.
Baraza hilo limetupilia mbali malalamiko ya vyama vya upinzani dhidi ya matokeo ya uchaguzi huo.