Didier Drogba kulishtaki gazeti la Daily Mail
15 Aprili 2016Matangazo
Gazeti maarufu la Uingereza la Daily Mail lilisema kuwa pauni 14,000 tu kati ya pauni milioni 1.7 zilizotolewa na wahisani kwa wakfu wa Didier Drogba zimetumika kuwanufaisha watoto nyumbani kwao Cote d'Ivoire.
Tume ya inayoshughulika na mambo ya hisani nchini Uingereza imesema inachunguza shughuli za wakfu huo ulioanzishwa mwaka wa 2009 na aliyekuwa mchezaji huyo wa Chelsea.
Drogba mwenye umri wa miaka 38, anayechezea klabu ya Montreal Impact ya Ligi Kuu ya Kandanda ya Canada, amekanusha tuhuma hizo katika taarifa yenye maneno mazito ambayo amesema habari hizo za Daily Mail ni za kumchafulia jina.
Mwandishi: Bruce Amani/AFP/DPA/AP
Mhariri: Yusuf Saumu