DOHA: Al-Jazeera inatangaza habari saa 24 kwa Kingereza
16 Novemba 2006Matangazo
Stesheni ya televisheni ya Al Jazeera yenye makao yake Doha,nchini Qatar,imeanzisha matangazo ya habari kwa lugha ya Kingereza.Kwa mujibu wa Al-Jazeera,vipindi vya habari vitakavyotangazwa kwa saa 24,sasa vinaweza kutazamwa na watu milioni 80 kwenye televisheni kupitia sateliti na kebo, hasa katika nchi za Mashariki ya Kati na Ulaya.Idara ya Kingereza ya Al-Jazeera ina vituo vyake vya matangazo katika miji ya Kuala Lumpur, London,Washington na Doha.