1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Dortmund yapanda kileleni

2 Novemba 2013

Ligi ya Ujerumani Bundesliga imeanza mchezo wake wa 11 jana Ijumaa(01.11.2013) ambapo makamu bingwa wa ligi hiyo Borussia Dortmund imeikaribisha nyumbani VFB Stuttgart.

https://p.dw.com/p/1AASX
DORTMUND, GERMANY - NOVEMBER 01: Sokratis (C) of Dortmund celebrates after scoring his team's first goal with team mates during the Bundesliga match between Borussia Dortmund and VfB Stuttgart at Signal Iduna Park on November 1, 2013 in Dortmund, Germany. (Photo by Sascha Steinbach/Bongarts/Getty Images)
Wachezaji wa Borussia Dortmund wakirudi kati baada ya kupachika bao dhidi ya StuttgartPicha: Getty Images

Ilikuwa karamu ya magoli kwa Borussia Dortmund makamu bingwa wa ligi ya Ujerumani , Bundesliga , baada ya kuisambaratisha VFB Stuttgart kwa mabao 6-1 katika uwanja wao wa Signal Iduna Park mjini Dortmund jana Ijumaa.

Mshambuliaji Robert Lewandowski alipachika mabao matatu katika kipindi cha pili wakati Borussia Dortmund ikijiweka kileleni mwa msimamo wa ligi, licha ya kuwa ni kwa muda tu, wakati ambapo mabingwa Bayern Munich watakuwa uwanjani hii leo(02.11.2013) kupambana na Hoffenheim, mchezo ambao huenda ukairejesha timu hiyo ya kutoka jimbo la Bavaria kileleni mwa msimamo wa ligi ya Ujerumani.

Borussia Dortmund's Robert Lewandowski celebrates a goal against Stuttgart during the German first division Bundesliga soccer match in Dortmund November 1, 2013. REUTERS/Ina Fassbender (GERMANY - Tags: SPORT SOCCER) DFL RULES TO LIMIT THE ONLINE USAGE DURING MATCH TIME TO 15 PICTURES PER GAME. IMAGE SEQUENCES TO SIMULATE VIDEO IS NOT ALLOWED AT ANY TIME. FOR FURTHER QUERIES PLEASE CONTACT DFL DIRECTLY AT + 49 69 650050
Nyota wa mchezo Robert LewandowskiPicha: Reuters

Mfungaji bora

Mshambuliaji huyo raia wa Poland ambaye hivi sasa anaongoza kwa kufunga mabao tisa katika Bundesliga , alifunga mabao matatu katika muda wa dakika 18 na kuisaidia timu yake kufikisha points 28, mbili mbele ya mabingwa Bayern Munich.

Stuttgart ambayo imepata kipigo chake cha kwanza katika michezo minane ya ligi chini ya kocha wao mpya Thomas Schneider , ilipata bao la kuongoza mapema katika mchezo huo wakati Karim Haggui alipouweka wavuni mpira wa kona uliopigwa na Alexandru Maxim lakini furaha hiyo haikudumu.

Dortmund ambayo itakuwa mwenyeji wa Arsenal London katika Champions League wiki ijayo, ilijibu haraka kwa kufunga mabao mawili ya haraka katika muda wa dakika tatu baada ya kuisambaratisha sehemu ya ulinzi ya Stuttgart kwa kasi yao.

Leo(02.11.2013) Bayer Leverkusen ambayo iko katika nafasi ya tatu, inapambana na Eintracht Braunschweig.

Hamburg SV ina kibarua dhidi ya Borussia Moenchengladbach, na Eintracht Frankfurt ina miadi na Wolfsburg. Katika kinyang'anyiro cha timu zilizo katika nafasi ya chini ya msimamo wa ligi Nüremberg ambayo hadi sasa haijapata ushindi inapambana na Freiburg. Kesho Jumapili ni zamu ya Augsburg ikitiana kifuani na Mainz na Bremen itaoneshana kazi na Hannover.

Ashindwa kutikisa wavu

Katika ligi ya Uhispania , FC Barcelona ilipata ushindi wa jasho pale ilipofanikiwa kuutikisa wazu wa Espanyol mara moja tu katika dakika 90 jana Ijumaa na kuendelea kuwa juu ya msimamo wa ligi hiyo. Messi anapitia kipindi chake kigumu kabisa katika soka baada ya kushindwa kutikisa nyavu katika ligi ya Uhispania tangu mwezi Septemba.

Barcelona's Argentinian forward Lionel Messi gestures during UEFA Champions League semi final first leg football match between FC Bayern Munich and FC Barcelona on April 23, 2013 in Munich, southern Germany. AFP PHOTO / PIERRE-PHILIPPE MARCOU (Photo credit should read PIERRE-PHILIPPE MARCOU/AFP/Getty Images)
Messi hajaziona nyavu tangu SeptembaPicha: PIERRE-PHILIPPE MARCOU/AFP/Getty Images

Nchini Ufaransa Paris Saint-Germain ilipata ushindi wa kishindo´ wa mabao 4-0 dhidi ya Lorient jana Ijumaa wakati Edinson Cavani akipachika mabao mawili na kuisaidia timu hiyo kuendelea kubaki kileleni mwa League 1.

Katika Premier League kocha Andre Villas-Boas wa Tottenham Hot Spurs amewaonya wachezaji wake kuwa hatakubali kuteleza tena iwapo timu hiyo inataka kuwamo katika mbio za kuwania ubingwa wa Premier League.

[39246694] Napoli vs. InterMilan epa03689034 Napoli Edinson Cavani celebrates after he scores the 3:0 goal, during the Serie A soccer match Napoli vs InterMilan at san Paolo stadium in Naples, Italy, 05 May 2013. EPA/CIRO FUSCO +++(c) dpa - Bildfunk+++
Edinson CavaniPicha: picture-alliance/dpa

Spurs inakumbana na Everton siku ya Jumapili.

Lakini shughuli inaikabili Arsenal wakati itakapoikaribisha Liverpool leo uwanjani Emirates. Fulham inapambana na Manchester United, Hull City ina miadi na Sunderland, Manchester City inaikaribisha Norwich City , wakati Newcastle ina kibarua na Chelsea.

epa02789384 (FILE) A file picture dated 07 April 2011 shows FC Porto's head coach Andre Villas-Boas giving instructions to his players during the UEFA Europa League quarter-final, 1st leg match against FC Spartak Moscow at Dragao Stadium in Porto, Portugal. Andre Villas-Boas was appointed Chelsea FC manager, the English Premier League club said on 22 June 2011. Villas-Boas signed a three-year contract and will start working immediately after resigning as FC Porto coach on 20 June. EPA/FERNANDO VELUDO *** Local Caption *** 00000402674371 +++(c) dpa - Bildfunk+++
Kocha wa Spurs André Villas-BoasPicha: picture alliance/dpa

Pambano lingine la kuvutia kesho Jumapili mbali ya Everton na Spurs ni pambano la kwanza la watani wa jadi kusini mwa Wales katika premier league msimu huu ambapo Swasea inasafiri kwenda Cardiff.

Mwandishi : Sekione Kitojo / afpe / rtre

Mhariri: Bruce Amani