1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

DRC: Idadi ya waliofariki kwa Ebola yaongezeka

12 Septemba 2014

Shirika la afya ulimwenguni,WHO limesema idadi ya watu waliofariki kutokana na ugonjwa wa Ebola nchini Kongo imeongezeka mara dufu na kufikia 62 kwa kipindi cha wiki moja iliopita.

https://p.dw.com/p/1DBGU
Picha: picture-alliance/dpa/C. Van Nespen

Hata hivyo shirika la WHO limesema ugonjwa huo umebaki kwenye eneo moja pekee huko Djera ,jimboni Equateur. Changa moto kubwa hivi sasa ni kampeni ya kuhamasisha wakaazi wa maeneo hayo ambapo baadhi ya wanaougua wanajificha,limelezea shirika la madaktari wasiokuwa na mipaka,MSF. Kamati ya pamoja ya madaktari wa Kongo,na wale wa mashirika ya kimataifa imezidisha huduma kwa wagonjwa na watu waliowasiliana na wagonjwa hao mnamo kipindi cha wiki tatu iliopita.Taarifa kamili na mwandishi wetu Saleh Mwanamilongo. Kusikiliza ripoti hiyo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.

Mwandishi: Salehe Mwanamilongo

Mhariri: Saumu Yusuf

Ruka sehemu inayofuata Gundua zaidi

Gundua zaidi